JUMANNE FEBRUARI 23
Tuliamka saa kumi na moja asubuhi. Tulikuwa katika shamba. Kulikuwa kunapendeza sana. Baada ya kiamsha kinywa tulirekodi watoto wakijiandaa kuenda shuleni. Tulienda nao hadi shuleni na kuendelea kurekdi wakiwa huko. Niliulizwa maswali na wanafunzi wengine juu ya maisha ng'ambo na kwanini tuna tengeneza filamu. Watoto hao walikua watiifu sana.
Ilipofika saa nne hivi tulishuhudia mbuzi akichinjwa. Tulishtuka sana na mimi na Winston tulisimama tumepigwa na bumbuwazi, tukisikia mlio wa mbuzi huyo. Hatukuwai kushuhudia kisa kama hicho. Jionee picha mwenyewe.
Baada ya Joshua na Nguguye kupanga bajeti ilikuwa wakati wa kuchoma mbuzi huyo.
Kulikuwa na joto kali. Nyama ya mbuzi ilikua ndani ya ndoo. Nzi wengi walizunguka nyama. Nyama zikawekwa ju ya jiko na kuchomwa. Joshua aliku mpishi akigeuza nyama kila upande. Alinipa kidogo nionje, nikaitafuna na kitu kilivunjika mdomoni. Mdomo wangu ulijaa ladha ya nyama na maini. Winston alikua bado katika hali ya mshtuko kwa kuona mbuzi akichinjwa. Si rahisi kuzoea vile wanatengeneza nyama lakini nilifurahi vile wao walifurahia.

Skriv en kommentar