Ijumaa, Machi 12
Kama Kawaida, Joshua alibisha mlangoni mwangu saa kumi na moja asubuhi. Kichwa kilikua kinaniuma. Leo nilikua niamke, nile kiamsha kinywa, ni fanye mazoezi, nisafishe, nifagie, nioga na nijitayarishe kwa kazi ya filamu. Winston alikuwa tayari amewasili mahala pa kupigia filamu ya leo. Changamoto nilioona isio ya kawaida ni kwamba nitapigia mswaki asubuhi na nijioni huko akamba handicraft. Harufu kutoka kwa choo na bafu ya mahala ninapoishi hunifanya kuhisi mgonjwa.

Nasikia kuchoka. Mwili umejaa uchovu lakini pia niko na motisha. Leo nimesumbuliwa na nimechoka. Naona haya kukubali nimechoka kwasababu nataka niwe na uwezo wa kushughulikia kila kitu, niwe mwenye nguvu na uvumilivu. Najiona kama ndege ambae anawaeleza watu zaidi mia moja ninaokutana nao kilia siku nini ninafanya na kwanini. Nimechoshwa na watu kwa njia kuniita mzungu. Naumia kwasababu ya kuona umaskini na shida ya wakenya. Uchungu moyoni haushi na huzuni imenijaa. Poleni wakenya kwa matatizo yenu. Sasa nahisi kama ni ndugu zangu na siwezi kuwaacha wakiteseka. Leo niliku na donda la koo kwa kushuhudia haya lakini lazima nitimize nilichokusudia kufanya. Hisia zangu zinanieleza kwamba siku moja nitwasaidia hawa. Nimetamani niwe na familia yangu, nile chakula cha mamangu. Nawapa hongera nyie mnaoishi kwa shida ya harufu mbaya, uchafu, joto, ajali barabarani umaskini, hasira, utamaduni usioleta maendeleo na ufisadi. Na yote haya kwasababu hamna nafsi nyingine.

Nitakuja nyumbani usiku. Majirani wangu huwa wamekaa katika yadi. Mimi nitajiunga nao. Huruma yao, upendo na udadisi unanitia nguvu. Kuona dunia katika macho yao ni shida, lakini jamii yao, jinsi ambavyo wanahudumiana.

Skriv en kommentar