Jumapili, 21 Machi


Askari wawili na bunduki walikuja kwa gari letu. Tuliongea na dereva wetu aongee nao kwasababu mwili wangu ulikua mchovu sana. Askari hao walitaka pesa ili kuturuhusu kuingia mahali hapo. Tulikua hatujabeba pesa zozote kwasababu tulikua tumezoea kulipa na kadi ya benki. Askari walituambia eti ni lazima turudi Nairobi tuchukue pesa halfu ndio turudi. Nilikasirika sana na tukaanza kubishana na askari hao. Mwishowe dereva wetu ndie aliongea nao na wakaturuhusu tuingie Masai Mara.


Masai Mara ni pahala pazuri mno. Wanyama ni wengi na wanazurura kila mahali. Jioni hiyo tulisherehekea kwa mvinyo na chakula.


Siku iliyopita niliozwa kwa dereva wetu wa kimasai. Tulipokua tunakula chakula cha jioni, alitaka kutumia wazazi wangu ng'ombe 40 na matandikio ya kitanda. Nilijaribu kumweleza kua sio lazma, Winston nae alikataa hivyo na akaiambia kua hivyo ndivyo inavyofaa.
Jumatatu saa kumi na moja tulirauka na kuanza safari yetu kuelekea Nairobi. Huko Nairobi tuko na mahojiano muhimu.



Skriv en kommentar