Jumanne, Machi 16
Ilhali sisi hufanya kazi masaa ishirini kila siku, saa zingine sisi hukaa na kuongea ju ya yale tunayoyaona na kupitia hapa. Wakati mmoja, Anette alikua na maoni haya:

"Ni kama kuna mstari inayotutofautisha sisi (wazungu) na wakenya. Najaribu sana kuonyesha kama sioni haya matatizo. Mimi nina shibe na nguo safi. Na kuna watoto wadogo nawaona na nguo zilizoraruka na chafu. Kuna taka kila mahali, na nyumba zimejengwa kwa udongo na mabati. Wanakaa kama hawana usaidizi wowote. Hii sii haki. Maisha yao imenifanya nione kama natoka kutoka dunia tofauti"

Siku chache zilikua zimebaki na singeweza kulipia chakula hotelini ama kuenda kujifurahisha kwa kilabu. Sikuweza kununua hata nguo ama chochote ninachokihitaji. Lakini tarehe 25, pesa iliingia kwa akaunti yangu, na nikaweza kununua vitu nilivyohitaji na kulipa madeni. Mbeleni, sikuelewa maisha yanaweza kua hivi.
Anette: "Huko ng'ambo nina nyumba iliyo safi na yakupendeza. Nina friji iliyojaa vyakula vingi, nina bafu kubwa iliyo na maji safi inayotoka kwa mferiji. Lakini kwa nyumba ya Rose ya kiswahili, ana sahani moja, na hamna maji kwa bafu. Maji inanunuliwa kwa mitungi na ni ghali sana. Nikiangalia vile Rose anaishi, vile ambavyo majirani wake wanaishi watu hata saba kwa chumba moja ndogo, naona masikitiko sana. Hata watu wakiniambia nafaa kuishi kwa matajiri, naona ni kweli. Kuona umaskini wa hali hii umenitatiza sana. Nimekua nikiona kwa runinga lakini kamwe sikua nimeona na macho yangu."

"Najua pesa, nguo na vitu vya duniani sio kila kitu maishani. Najua sasa kwamba mapenzi na urafiki ni bora kuliko chochote kengine. Lakini kwangu mie, sio pesa ama nguo ambayo ndio shida. Shida yangu ni kupenda starehe. Serikali ya nchi hii imeshindwa kuwalinda watu wao kutoka umaskini. Macho yangu imefunguliwa. Najiona ni kama nimelindwa na wavu ya usalama na sina matatizo ya maisha. Nikifikiria watu wanoishi na Rose, naona kweli hawana mlinzi wa kuwachunga, hawana wavu wa usalama."

Skriv en kommentar