Nitawacha Winston aendelee na Hadithi:


Ijumaa 19 Machi


Mwanamke aliyetuwekea viti vya basi alituuliza "Mna hakika mnataka kutumia basi?". Alikua kama mama aliye na wasiwasi kwasababu ya watoto wake. Wakati huo nilikua nimechoka na joto na nilitaka tu tuondoke.


Mlipuko ulinamsha saa tisa za asubuhi. Nilikua nimelala huku nikiegeza kichwa kwenye kioo cha basi. Mlipuko ulipotokea, nilisikia glasi ziniangukia kwa nyuso. Sikuelewa kilichokua kinatendekea. Nilikua nimeshtuka huku nikiona shimo kwa kioo cha basi. Nilijiangalia mwili kama nilikua nimeumizwa kokote, mara nikaskia Rose na Anetten wakiniambia " weka kichwa chini Winston". Nilijirusha chini ju ya glasi ziliokua zimenguka chini. Dereva wa basi naye akapeleka basi kwa kasi ili kuondoka mahali hapo.


Nilikaa chini kwa dakika chache alafu nikasongea mahali Rose na Annette walikua wamekaa. Nilishangaa vile watu wengine kwa basi waliku watulivu ni kama hakuna kilichotendeka.
Haikuwa mpaka jioni tulipokua Masai Mara ambapo nilielewa kilichotendeka. Dereva wetu alitueleza kwamba ilikua ni watu wanajaribu kuiteka nyara basi hio. Sikua bado naweza kuamini kwamba niliku karibu na kupigwa risasi. Nilinyamaza huku nikivumta pumzi na kushukuru kwa mashia niliyo nayo.


Skriv en kommentar