Mombasa ni jiji la pili kubwa nchini Kenya. Ni jiji lililo na bandari ya Kenya na huwa na watalii wengi. Watu wengi huku ni waislamu na watu wa asili ya kimijikenda. Mombasa ni jiji lenye joto na kuzuri sana. Watu wengi huvutiwa na mahala hapa.
Wakamba ni baadhi ya makabila waliokuja hap kufanya kazi ya uchongaji wa mbao. Wengi wao wameacha familia zao huko bara na wamekuja kufanya kazi mjini.
Tuliopfika Mombasa, nilishangazwa na joto iliopo hapa. Huko wamunyu hali ya anga ilikua ya baridi. Ilikua ni usiku lakin joto ilikua nyingi kupindukia, takriban nyuzi 30. Niliogopa kufikiria joto itakuaje mchana ukifika. Hata wakaazi wa hapa walikua wanalalamika ju ya joto.
Hoteli yetu ilikua katikati mwa mji wa Mombasa. Nilivyokaa ndani ya gari nilitamani upepo. Lakini baadaya kuingia hotelini nilipata kipepeo cha stima ambayo niliwakisha kwa haraka. Sisi tutakaa hapa hotelini lakini Rose atakaa chaani.
Skriv en kommentar